Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Februari: Wahubiri wanaweza kutoa mojawapo ya vitabu vifuatavyo: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Je, Kuna Muumba Anayekujali?, na Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia kwenye ziara ya kwanza. Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki na hakubali funzo la Biblia, mhubiri anaweza kumwachia magazeti yoyote ya zamani au broshua inayomfaa. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mwenye nyumba akipendezwa, mpe trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Unapowarudia watu waliohudhuria Ukumbusho na/au mikutano na makusanyiko, lakini hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida, zingatia kuwaachia kitabu Biblia Inafundisha.
◼ Hotuba ya pekee itatolewa wakati wa mwisho-juma utakaofuata Ukumbusho na ina kichwa “Je, Mwisho Uko Karibu Zaidi Kuliko Unavyofikiri?”
◼ Iwapo unapanga kutembelea nchi ambayo haijaorodheshwa katika ripoti ya utumishi ya mwaka huu au anwani yake haijaonyeshwa kwenye ukurasa wa mwisho wa Kitabu cha Mwaka cha karibuni zaidi, tafadhali wasiliana na ofisi yenu ya tawi ili ujue hatua za tahadhari unazopaswa kuchukua au maagizo hususa unayohitaji kufuata. Huenda ikawa kazi ya Ufalme katika eneo hilo imewekewa vizuizi. (Mt. 10:16) Katika nchi fulani huenda lisiwe jambo la busara kwa wageni kuwasiliana na Mashahidi wenyeji au makutaniko. Huenda ofisi ya tawi itakupa pia mwelekezo kuhusu mahubiri yasiyo rasmi au kubeba vitabu. Ukifuata mwelekezo unaotolewa utaepuka mambo mengi yanayoweza kukuletea matatizo au kuathiri kazi ya Ufalme katika nchi unayotembelea.—1 Kor. 14:33, 40.