Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha mafunzo ya Biblia katika Jumamosi ya kwanza mwezi wa Machi
“Watu wengi husherehekea kuzaliwa kwa Yesu, lakini je, unafikiri ni muhimu kukumbuka kifo cha Yesu?” Mruhusu ajibu, kisha umpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 1, na mzungumzie habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 na msome angalau andiko moja. Fanya mpango wa kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Machi 1
“Kuna makanisa mengi na madhehebu mengi yenye mafundisho na mazoea tofauti-tofauti. Unafikiri kila mtu anayejidai kuwa Mkristo anatenda jinsi Mkristo anavyopaswa kutenda? [Mruhusu ajibu.] Yesu alisema kwamba hii ni mojawapo ya alama zinazowatambulisha Wakristo wa kweli. [Soma Yohana 13:34, 35.] Gazeti hili linazungumzia mambo matano ambayo Yesu alisema, na ambayo yanatusaidia kuwatambulisha wafuasi wake wa kweli.”
Amkeni Machi
“Tunazungumza na majirani zetu kuhusu tabia fulani inayokera. Inaonekana kwamba watu siku hizi wana hasira sana na wanakasirika upesi. Unafikiri ni nini kinachosababisha hilo? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Biblia inasema kuhusu hasira. [Soma Zaburi 37:8.] Gazeti hili linazungumzia baadhi ya sababu zinazowafanya watu wazidi kuwa na hasira leo na jinsi tunavyoweza kudhibiti hasira yetu.”