Maajabu ya Uumbaji Yanafunua Utukufu wa Mungu
Watu wengi wanafurahia kutazama uumbaji. Lakini ni wachache tu wanaotambua kwamba uumbaji unafunua fikira na hisia za Muumba wetu Mkuu. (Rom. 1:20) Zamani za kale, Daudi alijifunza kumhusu Yehova kupitia Neno Lake takatifu. Pia ‘alimwona’ na kumkaribia Yehova kupitia uumbaji. (Zab. 8:3, 4) Video yenye kichwa Maajabu ya Uumbaji Yanafunua Utukufu wa Mungu imekusudiwa kutusaidia sisi, watoto wetu, na wanafunzi wa Biblia kuchunguza kwa makini uumbaji wa Yehova. Pia inatusaidia kuona sifa za Muumba wetu Mkuu, na hivyo kumkaribia zaidi. Baada ya kuitazama video hii, ona kama unaweza kujibu maswali haya yafuatayo.
(1) Ukubwa na mpangilio wa anga unaongezaje uthamini wako kwa Yehova? (Isa. 40:26) (2) Tunapoyatazama maji kwa makini, tunajifunza nini kumhusu Mungu? (Ufu. 14:7) (3) Ukubwa wa dunia, na umbali kati yake na jua unaonyeshaje hekima ya Yehova? (4) Mwezi uliumbwa kwa kusudi gani? (Zab. 89:37) (5) Yehova alimwumba mwanadamu jinsi gani ili afurahie maisha? (6) Chembe za DNA ni nini? (Zab. 139:16) (7) Mwanadamu ni tofauti na viumbe vingine duniani kwa njia zipi? (Mwa. 1:26) (8) Unatazamia nini katika ulimwengu mpya?
Mambo ya Ziada: (9) Rangi hutokea jinsi gani? (10) Kupitia nguvu za uvutano, ni nini kinachotokea katika miti ili maji yapande kutoka kwenye mizizi mpaka juu? (11) Maji yana umuhimu gani katika mwili wetu? (12) Toa mifano inayoonyesha ushirikiano uliopo kati ya viumbe hai. (13) Viumbe vinajua namna gani jinsi ya kushirikiana na viumbe vingine? (14) “Pembe bora” ni nini, na inaonekanaje katika uumbaji?
‘Angalieni kwa Makini’ Uumbaji wa Yehova: Yesu alitutia moyo ‘tuangalie kwa makini ndege wa mbinguni’ na ‘kujifunza kwa mayungiyungi ya shamba.’ (Mt. 6:26, 28) Kufanya hivyo kunaweza kuimarisha imani yetu na kutufanya tumtumaini zaidi Yehova. Pia kutatusaidia kuthamini hekima yake, uwezo, na upendo wake. Tuwe na bidii na tutenge wakati wa kuchunguza maajabu ya uumbaji wa Yehova badala ya kukengeushwa na kazi za ulimwengu huu. Tutafakari yale ambayo uumbaji unafunua kumhusu Mungu wetu.—Zab. 19:1.