Ratiba ya Juma Linaloanza Machi 26
JUMA LINALOANZA MACHI 26
Wimbo 92 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 18 ¶12-18 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yeremia 12-16 (Dak. 10)
Na. 1: Yeremia 13:1-14 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Ni Nani Wanaopaswa Kula Mkate na Kunywa Divai Wakati wa Mlo wa Jioni wa Bwana?—rs uku. 338 ¶3-4 (Dak. 5)
Na. 3: Ukumbusho Unapaswa Kuadhimishwa Mara Ngapi na Wakati Gani?—rs uku. 339 ¶3–uku. 340 ¶1 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo. Julisha kutaniko kuhusu maeneo ambako bado tunahitaji kusambaza mialiko ya Ukumbusho.
Dak. 10: Msisahau Ukaribishaji-Wageni. (Ebr. 13:1, 2) Hotuba itolewe na mzee. Taja mipango ya Ukumbusho ya kutaniko lenu. Toa mapendekezo ya jinsi kila mhubiri anavyoweza kuonyesha ukarimu kwa wageni na kwa wahubiri wasiotenda watakaohudhuria Ukumbusho. Panga kuwe na onyesho fupi lenye sehemu mbili. Katika sehemu ya kwanza ya onyesho, mhubiri anamkaribisha kabla ya mkutano kuanza mtu aliyepata mwaliko. Na katika sehemu ya pili ya onyesho, mhubiri anafanya mipango baada ya mkutano kukutana na mtu huyo tena.
Dak. 20: “Maajabu ya Uumbaji Yanafunua Utukufu wa Mungu.” Maswali na majibu. Tumia habari iliyo katika fungu la kwanza na la mwisho kwa ajili ya utangulizi mfupi na umalizio mfupi. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi walivyonufaika kwa kutazama video hiyo. Zungumzia jinsi video hiyo inavyoweza kutumiwa katika huduma. Katika maeneo ambayo video hii haipatikani, zungumzeni sehemu “Sayari Yenye Uhai Tele” katika broshua Uhai—Ulitokana na Muumba? ukurasa wa 4-10 na utumie maswali ya pitio ili kukazia mambo muhimu.
Wimbo 110 na Sala