Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki na hakubali funzo la Biblia, mhubiri anaweza kumwachia gazeti lolote la zamani au broshua yoyote inayomfaa. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa, zungumzia trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Unapowarudia watu waliohudhuria ukumbusho au mikutano na makusanyiko, lakini hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida, jitahidi kuanzisha funzo ukitumia kitabu Biblia Inafundisha. Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki na hakubali funzo la Biblia, mhubiri anaweza kumwachia gazeti la zamani au broshua yoyote ambayo inayomfaa.
◼ Ukumbusho utaadhimishwa Alhamisi, Aprili 5, 2012. Ikiwa kutaniko lenu hufanya mikutano siku ya Alhamisi, mnapaswa kufanya mikutano hiyo siku nyingine katika juma hilo. Iwapo Jumba lenu la Ufalme linatumiwa na makutaniko kadhaa na haiwezekani kufanya mikutano siku nyingine, sehemu zinazohusu hasa kutaniko lenu, zizungumziwe katika Mkutano mwingine wa Utumishi.
◼ Video za Young People Ask—How Can I Make Real Friends? na Young People Ask—What Will I Do With My Life?, zitazungumziwa katika Mikutano ya Utumishi inayofuata. Ikiwa kutaniko lenu linahitaji video hizo, ziagizeni haraka iwezekanavyo.