Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha mafunzo ya Biblia katika Jumamosi ya kwanza mwezi wa Aprili
“Ubatizo ni zoea la kawaida miongoni mwa Wakristo wengi. Wewe unaonaje, ubatizo ni muhimu? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inazungumzia mambo yanayofaa kufikiriwa kuhusu ubatizo.” Mpe mwenye nyumba toleo la Aprili 1 la Mnara wa Mlinzi, na pitieni pamoja habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16, na angalau andiko moja. Mtolee magazeti na upange kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Aprili 1
“Watu wana maoni mbalimbali kumhusu Yesu. Baadhi yao wanafikiri kwamba alikuwa Masihi aliyeahidiwa. Wengine wanafikiri alikuwa mtu mzuri tu. Wengine nao wanafikiri kwamba hakuwepo kamwe. Wewe unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na Biblia ni muhimu kujua ukweli kumhusu Yesu. [Soma Yohana 17:3.] Gazeti hili linaonyesha majibu ya Biblia ya maswali ambayo watu wengi huuliza kumhusu Yesu.”
Amkeni! Aprili
“Je, unakubaliana nami kwamba familia zinakumbwa na matatizo mengi leo? [Mruhusu ajibu.] Familia zinaweza kupata ushauri unaofaa katika Biblia. Ona jinsi andiko hili linavyosema. [Soma Zaburi 119:105.] Gazeti hili linazungumzia jinsi familia zenye wazazi wa kambo zinavyoweza kufanikiwa kushughulikia matatizo kwa kufuata kanuni za Biblia.”