Ratiba ya Juma Linaloanza Aprili 9
JUMA LINALOANZA APRILI 9
Wimbo 123 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 19 ¶1-5, masanduku kwenye uku. 149-150 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yeremia 22-24 (Dak. 10)
Na. 1: Yeremia 23:15-23 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Kwa Nini Maisha Katika Ulimwengu Mpya Hayatachosha? (Dak. 5)
Na. 3: Kutumia Ushauri wa Biblia Kunaweza Kuboresha Ndoa—rs uku. 231 ¶5-8 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 15: Nufaika na Kitabu cha Mwaka—2012. Tumia “Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza” ikiwa msingi wa hotuba ya utangulizi. Kisha, waalike wasikilizaji wasimulie mambo yaliyowapendeza ambayo wamesoma katika “Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita.” Halafu, waombe watoe maelezo kuhusu mambo yenye kupendeza ya ripoti ya ulimwenguni pote. Malizia kwa kuwatia moyo wote wamalize kusoma Kitabu cha Mwaka.
Dak. 15: “Mapendekezo Matatu ya Kuboresha Ufundishaji Wako.” Maswali na majibu. Panga onyesho la mhubiri akizungumzia na mwenye nyumba habari iliyo kwenye ukurasa wa 3 fungu la kwanza katika kitabu Biblia Inafundisha. Baada ya mhubiri kusoma sehemu ya andiko la Ayubu 10:15 iliyonukuliwa, anatumia dakika moja hadi mbili akieleza kuhusu Ayubu. Onyesho hilo lifanywe mnapozungumzia fungu la 2. Baada ya onyesho, waulize wasikilizaji kwa nini hiyo haikuwa njia nzuri ya kufundisha, hata ingawa mambo aliyoeleza kuhusu Ayubu yalikuwa sahihi.
Wimbo 10 na Sala