Ratiba ya Juma Linaloanza Aprili 23
JUMA LINALOANZA APRILI 23
Wimbo 45 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 19 ¶12-20, sanduku kwenye uku. 152 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yeremia 29-31 (Dak. 10)
Na. 1: Yeremia 31:15-26 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Je, Mungu Anawatazamia Wakristo Washike Sabato ya Kila Juma? (Dak. 5)
Na. 3: Je, kwa Kweli Maria Alikuwa Bikira Alipomzaa Yesu?—rs uku. 182 ¶1-2 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Matangazo. Tumia dakika moja au mbili kuzungumzia makala chache za magazeti ya karibuni zaidi yaliyo kutanikoni. Zungumzia makala ambazo huenda zikawavutia watu katika eneo lenu. Halafu, kwa kutumia makala za kwanza za Mnara wa Mlinzi, waombe wasikilizaji wapendekeze swali linaloamsha upendezi ambalo watauliza, na vilevile andiko ambalo watasoma. Fanya vivyo hivyo kuhusu makala za kwanza za Amkeni! na, wakati ukiruhusu, kuhusu makala nyingine moja katika mojawapo ya magazeti hayo. Panga onyesho la jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Dak. 15: “Faidika Kabisa na Funzo la Kibinafsi.” Maswali na majibu. Watie moyo wote watenge wakati hususa kwa ajili ya funzo la kibinafsi, kufanya utafiti, na kutafakari.
Dak. 10: “Mambo ya Kuzungumzia Wakati wa Ibada ya Familia.” Hotuba inayokazia habari iliyo kwenye sanduku lililo katika ukurasa wa 28 wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 2010. Mhoji kifupi mhubiri ambaye amewahi kutembelea ofisi ya tawi.
Wimbo 119 na Sala