Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha mafunzo ya Biblia katika Jumamosi ya kwanza mwezi wa Mei
“Je, unafikiri dini inachochea upendo na amani au chuki na jeuri? [Mruhusu ajibu.] Hebu nikuonyeshe jambo lenye kupendeza kuhusu habari hii.” Mpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi, la Mei 1, na mzungumzie habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 na msome angalau andiko moja. Mpe magazeti, kisha upange kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Watu wengi huamini kwamba ni sawa dini kujihusisha na mambo ya kisiasa, lakini wengine huhisi kwamba dini na siasa hazipaswi kuchanganywa. Wewe unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi Yesu alivyotenda watu walipotaka ajiingize katika siasa za siku hizo. [Soma Yohana 6:15.] Gazeti hili linaeleza ni kwa nini Yesu alitenda kwa njia hiyo na linazungumzia njia bora zaidi ambayo Wakristo wanaweza kuisaidia jamii.”
Amkeni! Mei
“Karibu kila mtu tunayezungumza naye ametendewa isivyo haki wakati fulani. Unafikiri kuna suluhisho la ukosefu wa haki? [Mruhusu ajibu.] Ona unabii huu kuhusu mtawala fulani ambaye atakomesha ukosefu wa haki. [Soma Zaburi 72:11-14.] Gazeti hili linazungumzia ahadi za Biblia kuhusu wakati ujao ambapo haki itatekelezwa.”