Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Kulikuwa na utendaji mzuri mwezi wa Novemba 2011 na wahubiri waliwaachia watu vitabu 52,984 na kuongoza mafunzo ya Biblia 45,374. Hivyo vilikuwa vilele vipya na idadi hiyo ya mafunzo ya Biblia ni karibu mara mbili ya idadi ya wahubiri. Jitihada zilizofanywa na wahubiri na mapainia za kuwapa watu wanaopendezwa baadhi ya machapisho ya zamani zilichangia idadi hiyo kubwa ya vitabu vilivyoachiwa watu mwezi wa Novemba.
Uganda: Jumla ya wahubiri 5,606 waliongoza mafunzo ya Biblia 15,144 katika mwezi wa Novemba 2011. Idadi hiyo ya wahubiri ni ongezeko la asilimia 8, na mafunzo ya Biblia yaliyoongozwa ni asilimia 10 zaidi ikilinganishwa na mwezi wa Novemba 2010. Kwa kweli, watu wa Yehova wanafanya kwa bidii kazi hii ya kufundisha inayookoa uhai!—1 Tim. 4:16.