Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Juni 25, 2012. Tarehe ambayo kila sehemu itazungumziwa imeonyeshwa ili wahubiri waweze kufanya utafiti kwa ajili ya shule kila juma.
1. Tunapata uhakikisho gani kutokana na kisa cha Yeremia kuokoka nyakati ngumu kiuchumi? (Yer. 37:21) [Mei 7, w97 9/15 uku. 3 fu. 4–uku. 4 fu. 1]
2. Wakristo wenye tumaini la kuishi Duniani huiga mfano mzuri wa Ebed-meleki katika njia zipi? (Yer. 38:8-13) [Mei 7, su uku. 179 fu. 9]
3. Kwa kuwa Yehova alitumia walinzi wa Nebukadreza kuwalinda Yeremia na Baruku, je, inafaa Wakristo watafute ulinzi wa maofisa wa polisi walio na silaha? (Yer. 39:11-14) [Mei 14, w84 8/1 uku. 23]
4. Mambo “makuu” ambayo huenda Baruku alikuwa akijitafutia ni nini, na kutii kwake shauri la Yehova kunatusaidia kukazia nini? (Yer. 45:5) [Mei 21, w06 8/15 uku. 18 fu. 2; uku. 19 fu. 6]
5. Yehova anapozungumzia hukumu za haki ambazo angeleta juu ya Edomu, kwa nini anajitofautisha na “wakusanya-zabibu” na “wezi”? (Yer. 49:9, 10) [Mei 28, w77-E uku. 442 fu. 7–uku. 443 fu. 1; si uku. 152 fu. 7, 8]
6. Tunaweza kujifunza nini kutokana na mambo yaliyompata Mfalme Sedekia ‘alipoanza kumwasi mfalme wa Babiloni’? (Yer. 52:3, 7-11) [Juni 4, w88 9/15 uku. 17 fu. 8; w81-E 4/1 uku. 13 fu. 3-4; uku. 14 fu. 6]
7. “Kiti cha miguu” cha Yehova ni nini na “kibanda” chake ni nini? (Omb. 2:1, 6) [Juni 11, w07 6/1 uku. 9 fu. 2]
8. Yeremia alimaanisha nini aliposema kwamba Yehova ‘angekumbuka na kuinama juu’ yake, na kwa nini hilo ni muhimu sana kwetu? (Omb. 3:20) [Juni 18, w07 6/1 uku. 11 fu. 3]
9. Kwa nini ni muhimu mtu ajifunze kuchukua nira ya mateso wakati wa ujana wake? (Omb. 3:27) [Juni 18, w07 6/1 uku. 11 fu. 5; w87 2/15 uku. 24 fu. 1]
10. Mfano wa Ezekieli unaweza kutusaidiaje kusema kwa ujasiri licha ya kutopendezwa kwa wengine? (Eze. 3:8, 9) [Juni 25, w08 7/15 uku. 8-9 fu. 6-7]