Ratiba ya Juma Linaloanza Juni 25
JUMA LINALOANZA JUNI 25
Wimbo 63 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 22 ¶15-21 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Ezekieli 1-5 (Dak. 10)
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 20)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Matangazo. Panga onyesho la jinsi funzo la Biblia linavyoweza kuanzishwa katika Jumamosi ya kwanza mwezi wa Julai. Tumia magazeti ya karibuni zaidi mliyo nayo kutanikoni na nakala ya Huduma Yetu ya Ufalme iliyo na mapendekezo ya jinsi ya kutoa magazeti hayo.
Dak. 15: Tumia Wakati Wako kwa Hekima Unapokuwa Katika Huduma. (Efe. 5:15, 16) Mazungumzo yanayotegemea maswali yafuatayo. (1) Tunaweza kutumia wakati wetu kwa hekima jinsi gani (a) tunapoongoza mkutano wa utumishi wa shambani? (b) baada ya kumaliza mkutano wa utumishi wa shambani? (c) mhubiri fulani katika kikundi chetu anapozungumza kwa muda mrefu na mtu mwenye kupendezwa? (d) tunapolazimika kwenda mbali kutoka ziara moja ya kurudia hadi nyingine? (2) Tutaokoaje wakati ikiwa (a) tutahakikisha kwamba watu wa familia yetu wamekula, ikiwezekana, kabla ya mkutano wa utumishi? (b) kila mtu atafika mapema kwenye mkutano wa utumishi wa shambani? (c) tutamsikiliza kwa makini ndugu anayeongoza mkutano wa utumishi anapopanga vikundi na kuepuka kubadili mipango hiyo baada ya mkutano huo bila sababu maalumu? (d) kila mtu atajua mahali anapopaswa kuanza kuhubiri kabla ya kuondoka na kwenda kwenye eneo?
Dak. 10: Toleo la Mwezi wa Julai. Mazungumzo. Zungumzia yaliyomo katika machapisho yatakayotolewa mwezi wa Julai na upange onyesho moja au mawili.
Wimbo 29 na Sala