Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Julai
“Katika miaka ya karibuni, watu wamependa kujua zaidi kuhusu malaika. Unafikiri malaika ni viumbe halisi? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho gazeti hili linasema.” Mpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, na mzungumzie habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 na msome angalau andiko moja. Mpe magazeti na ufanye mipango ya kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
Soma Zaburi 65:2, kisha useme: “Watu wengi hukubali kwamba Mungu ndiye ‘Msikiaji wa sala,’ na wao husali kila siku. Lakini wengine hujiuliza, ‘Ikiwa kuna Mungu, kwa nini ulimwengu una matatizo mengi hivyo?’ Wewe unaonaje? Je, kuna Mungu ambaye husikia sala zetu? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jibu la Biblia kuhusu swali hili: ‘Kwa nini Msikiaji wa sala anaruhusu watu wateseke?’”
Amkeni! Julai
“Ikiwa ungeweza kubadili kitu kimoja kuhusu ulimwengu wetu, ungebadili nini? [Mruhusu ajibu.] Biblia inaonyesha ni kwa nini wanadamu hawana uwezo wa kuubadili ulimwengu wetu. [Soma Yeremia 10:23.] Gazeti hili linaeleza mambo ambayo Mungu anakusudia kubadili.”