Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Julai
“Watu wengi huyarudia maneno haya katika Sala ya Bwana: ‘Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.’ Unafikiri Ufalme huo ni nini? [Mruhusu ajibu.] Andiko hili la Biblia linatufunulia habari fulani.” Soma Danieli 2:44, kisha umpe mwenye nyumba nakala ya Mnara wa Mlinzi wa Julai 1. Soma na uzungumzie habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16. Mtolee magazeti na upange kurudi ili mchunguze jibu la swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Kwa kuwa maisha ni mafupi na yamejaa matatizo, watu wengi hujiuliza kama hali zitaendelea hivi milele. Umewahi kujiuliza swali hilo? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatuahidi kwamba maisha hayataendelea hivi milele. [Soma Ufunuo 21:4.] Gazeti hili linazungumzia kusudi la Mungu kuhusu dunia na pia linaonyesha mambo ambayo tunaweza kufanya ili kufanya maisha yetu yawe yenye furaha hata sasa.”
Amkeni! Julai
Taja msiba unaozungumziwa katika vyombo vya habari, kisha useme: “Unafikiri kwa nini Mungu anaruhusu mambo kama hayo kutokea? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na Biblia, Mungu huwaonea huruma watu wanaoteseka. [Soma Kutoka 3:7.] Biblia hutueleza pia sababu zinazomfanya Mungu aruhusu kuteseka na kwamba hivi karibuni atakomesha kabisa mambo yanayowafanya watu wateseke. Gazeti hili linaeleza jambo hilo.”