Mapendekezo Kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza ya Mwezi wa Julai
“Unafikiri Mungu ana maoni gani kuhusu sala zetu? Je, unafikiri anazithamini au anazivumilia tu?” Mruhusu ajibu. Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, na mzungumzie habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mwachie magazeti, na ufanye mipango ya kurudi ili kuzungumzia swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Kwa kuwa Mungu ni mweza yote, je, unafikiri anapaswa kulaumiwa kwa mambo yote mabaya yanayotokea ulimwenguni? [Mruhusu ajibu. Kisha soma andiko la Yakobo 1:13.] Gazeti hili linaeleza kwa nini mambo mabaya hutokea, na mambo ambayo Mungu atafanya ili kukomesha uovu na kuteseka.”
Amkeni Julai
“Wakati fulani maishani, karibu kila mmoja wetu hukabili aina fulani ya msiba, kama vile misiba ya asili, ugonjwa mbaya sana, au kifo cha mpendwa wetu. Tunapokabili mambo hayo, je, unafikiri kwamba ni muhimu kuendelea kuwa na mtazamo unaofaa? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi wameona kwamba Biblia imewasaidia kukabiliana na misiba. [Soma Waroma 15:4.] Gazeti hili linaelezea jinsi Biblia inavyoweza kutusaidia tunapokabili misiba.”