Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Desemba
“Watu wengi wanatazamia kurudi kwa Yesu. Ikiwa Yesu angerudi, ungependa afanye jambo gani?” Mruhusu ajibu. Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 1 na mzungumzie habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau andiko moja. Mwachie magazeti, na ufanye mpango wa kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Desemba 1
“Maisha yamejaa shughuli nyingi sana siku hizi, hivi kwamba ni vigumu kufikiria kumhusu Mungu. Je, unafikiri Mungu ni muhimu katika maisha yetu? [Mruhusu ajibu.] Katika Mahubiri yake ya Mlimani yanayojulikana sana, Yesu alisema ili tuwe na furaha ya kweli tunahitaji kupenda mambo ya kiroho. [Soma Mathayo 5:3.] Gazeti hili linataja mambo matatu yanayoonyesha kwa nini tunahitaji Mungu.”
Amken!Desemba
“Baada ya kusikia au kusoma habari kutoka kwenye vyombo vya habari, wengi wetu tunakuwa na maoni tofauti-tofauti. Je, unafikiri habari tunazopokea ni sahihi na za kweli? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatutahadharisha kuhusu kuamini mambo tunayosikia. [Soma Ayubu 12:11.] Gazeti hili linatupa madokezo fulani yatakayotusaidia tupime mambo tunayosikia na kusoma.”