Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Desemba
“Tumewatembelea ili kuzungumzia kuhusu familia. Wazazi wengi wangefurahi kuwa na watoto wanaompenda Mungu. Je, unafikiri watoto wanapaswa kujifunza wenyewe kumpenda Mungu au wanapaswa kufundishwa na wazazi wao?” Mruhusu ajibu. Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, na mzungumzie pamoja habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau andiko moja lililoonyeshwa. Mwachie magazeti na ufanye mpango wa kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Desemba 1
“Tumewatembelea kwa muda mfupi ili kuzungumzia kumhusu Mungu. Watu wana maoni tofauti-tofauti kumhusu Mungu. Je, unafikiri watu wengi wanamwona Mungu kuwa nguvu zisizo na utu au wanamwona kuwa rafiki anayewajali kibinafsi? [Mruhusu ajibu.] Andiko hili linatueleza kuhusu uhusiano wetu pamoja na Mungu. [Soma Yakobo 4:8a.] Gazeti hili linazungumzia mambo matatu tunayoweza kufanya ili tumkaribie Mungu zaidi.”
Amkeni Desemba
“Tumewatembelea kwa muda mfupi ili kuzungumzia tatizo la afya linalowahangaisha wengi. Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni, mtu mmoja kati ya wanne ataathiriwa na ugonjwa wa akili, kama vile ugonjwa wa kushuka moyo, wakati fulani wa maisha yake. Je, unafikiri magonjwa ya akili yanazidi kuongezeka? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatuahidi kwamba, wakati ujao magonjwa na maumivu hayatakuwapo. [Soma Ufunuo 21:3, 4.] Gazeti hili linazungumzia mambo kadhaa tunayopaswa kujua kuhusu magonjwa ya akili.”