Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Desemba
“Wakati huu wa mwaka watu wengi humkumbuka Yesu. Kulingana na maoni yako, ni jambo gani kubwa ambalo Yesu alitimiza? [Mruhusu ajibu.] Ona kichwa cha makala hii kwenye ukurasa wa 16.” Mpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, na mzungumzie habari zilizo chini ya mojawapo ya vichwa vidogo na angalau mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mwachie magazeti na ufanye mipango ya kurudi ili mzungumzie swali lingine.
Mnara wa Mlinzi Desemba 1
“Watu wengi msimu huu hunaswa na pilikapilika za Krismasi. Kati ya mambo haya, unafikiri ni jambo gani ambalo ni sehemu muhimu zaidi ya pilikapilika hizo? [Mwonyeshe mwenye nyumba orodha inayopatikana kwenye ukurasa wa 3 na mruhusu ajibu. Kisha ufungue makala inayohusiana na jambo hilo na usome andiko la msingi.] Gazeti hili linazungumzia njia ambazo tunaweza kumkumbuka Yesu mwaka mzima na si wakati wa Krismasi tu.”
Amkeni! Desemba
“Tunawatembelea watu kwa sababu watu wengi huwa na mikazo na mifadhaiko. Je, umeona kwamba siku hizi watu hukosa subira haraka? [Mruhusu ajibu.] Baadhi ya watu huamini kwamba tunaishi katika kipindi chenye mikazo kilichotabiriwa kwenye andiko hili la 2 Timotheo 3:1. [Soma] Gazeti hili linaeleza kwa nini kukosa subira kuna madhara na linatoa mapendekezo ya jinsi tunavyoweza kuwa wenye subira zaidi.”