Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Septemba
“Watu wengi wanaamini kwamba siku moja Mungu atawahukumu kulingana na matendo yao. Je, unafikiri kwamba Siku ya Hukumu ni siku ya kutazamiwa kwa hamu au ya kuogopwa? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho gazeti hili linasema.” Mpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, na mzungumzie habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 kisha msome angalau andiko moja. Mpe magazeti na ufanye mipango ya kurudi ili kuzungumzia swali linalofuata.
Mnarawa wa Milinzi Septemba 1
“Katika sehemu nyingi ulimwenguni, wanawake hubaguliwa na kutendewa vibaya. Inasikitisha kwamba imani za kidini zimechangia jambo hilo. Unaonaje? Kweli Mungu anawajali wanawake? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi Biblia inavyowaagiza waume wawatendee wake zao. [Soma Waefeso 5:28, 29.] Gazeti hili linaonyesha mambo ambayo Biblia inafunua kuhusu jinsi Mungu anavyowaona wanawake.”
Amkeni! Septemba
“Watu wengi wanasema kwamba siku moja uhai duniani utakoma, labda kwa sababu ya vita vya nyuklia au msiba wa asili kama vile mawe ya angani au mabadiliko ya hali ya hewa duniani. Je, unafikiri makisio kama hayo ya mwisho wa dunia yana msingi wowote au ni ya kuwaziwa tu? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatoa ahadi hii yenye kufariji. [Soma Zaburi 37:29.] Gazeti hili linachunguza hali fulani ambazo watu wanasema kwamba zitasababisha mwisho wa dunia, na vilevile mambo ya hakika ambayo Biblia inasema kuhusu wakati ujao.”