Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/12 uku. 4
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 8/12 uku. 4

Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Septemba

“Watu wengi wanaamini kwamba siku moja Mungu atawahukumu kulingana na matendo yao. Je, unafikiri kwamba Siku ya Hukumu ni siku ya kutazamiwa kwa hamu au ya kuogopwa? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho gazeti hili linasema.” Mpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, na mzungumzie habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 kisha msome angalau andiko moja. Mpe magazeti na ufanye mipango ya kurudi ili kuzungumzia swali linalofuata.

Mnarawa wa Milinzi Septemba 1

“Katika sehemu nyingi ulimwenguni, wanawake hubaguliwa na kutendewa vibaya. Inasikitisha kwamba imani za kidini zimechangia jambo hilo. Unaonaje? Kweli Mungu anawajali wanawake? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi Biblia inavyowaagiza waume wawatendee wake zao. [Soma Waefeso 5:​28, 29.] Gazeti hili linaonyesha mambo ambayo Biblia inafunua kuhusu jinsi Mungu anavyowaona wanawake.”

Amkeni! Septemba

“Watu wengi wanasema kwamba siku moja uhai duniani utakoma, labda kwa sababu ya vita vya nyuklia au msiba wa asili kama vile mawe ya angani au mabadiliko ya hali ya hewa duniani. Je, unafikiri makisio kama hayo ya mwisho wa dunia yana msingi wowote au ni ya kuwaziwa tu? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatoa ahadi hii yenye kufariji. [Soma Zaburi 37:29.] Gazeti hili linachunguza hali fulani ambazo watu wanasema kwamba zitasababisha mwisho wa dunia, na vilevile mambo ya hakika ambayo Biblia inasema kuhusu wakati ujao.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki