Ratiba ya Juma Linaloanza Novemba 5
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 5
Wimbo 115 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 1 ¶1-7 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yoeli 1-3 (Dak. 10)
Na. 1: Yoeli 2:17-27 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Tunaweza Kutumiaje Kanuni Iliyo Kwenye Methali 22:3? (Dak. 5)
Na. 3: Tunaweza Kuonyeshaje Heshima kwa Tengenezo la Yehova?—rs uku. 301 ¶8-12 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Wanawake Wanaotangaza Habari Njema Ni Jeshi Kubwa. (Zab. 68:11) Mazungumzo yanayotegemea Kitabu cha Mwaka—2012, ukurasa wa 117, fungu la 2, hadi ukurasa wa 118, fungu la 2; na ukurasa wa 130, fungu la 1, hadi ukurasa wa 131, fungu la 3. Waombe wasikilizaji waeleze mambo waliyojifunza.
Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 10: Njia za Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa Novemba. Mazungumzo. Tumia dakika 30 hadi 60 kueleza kwa nini magazeti hayo yatawavutia watu katika eneo lenu. Kisha, kwa kutumia makala za kwanza za Mnara wa Mlinzi, waombe wasikilizaji wapendekeze swali linaloamsha upendezi ambalo watauliza, na pia andiko ambalo watasoma. Fanya vivyo hivyo kuhusu makala za kwanza za Amkeni! na, ikiwa wakati unaruhusu, zungumzia makala nyingine moja kutoka katika mojawapo ya magazeti hayo. Panga onyesho la jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Wimbo 105 na Sala