Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Novemba
“Wengi wetu tunapenda serikali nzuri. Unaonaje, ni serikali gani inayoweza kusuluhisha matatizo ya wanadamu? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho gazeti hili linasema.” Mpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, na mzungumzie habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 kisha usome angalau andiko moja. Mwachie magazeti, kisha upange kurudi ili mzungumzie swali linalofuata. Ikiwa hakuna matoleo ya Novemba, tumia magazeti ya karibuni mliyo nayo kutanikoni na mapendekezo ya jinsi ya kuyatoa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme iliyo na mapendekezo hayo.
Mnara wa mlinzi Novemba 1
“Tungependa kujua maoni yako. Ikiwa ungeweza kumwuliza Mungu swali, ungemwuliza swali gani? [Mruhusu ajibu] Kulingana na Yesu, ni jambo linalofaa kutafuta majibu ya maswali yetu ya unyoofu. [Soma Mathayo 7:7.] Gazeti hili linatoa majibu ya Biblia ya maswali haya matatu muhimu.” Mwonyeshe mwenye nyumba maswali yaliyo chini katika ukurasa wa 3.
Amkeni Novemba
“Leo tunawatembelea watu wote tukiwa na ujumbe kwa ajili ya familia. Imekuwa kawaida kuwa na familia za mzazi mmoja. Je, unafikiri zina matatizo zaidi kuliko familia zenye wazazi wawili? [Mruhusu ajibu.] Wazazi wengi wamepata mashauri yanayofaa katika Biblia. [Soma 2 Timotheo 3:16.] Gazeti hili linatoa baadhi ya mapendekezo ya kuwasaidia wazazi wasio na wenzi wafanikiwe kutimiza daraka lao zito.”