Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha mafunzo ya Biblia katika Jumamosi ya kwanza mwezi wa Novemba
“Je, unafikiri kwamba watu wanaojitahidi kumtii Mungu ni wenye furaha kuliko wengine? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili lina mambo yenye kuvutia kuhusiana na hilo.” Mpe mwenye nyumba nakala ya Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1. Soma na mzungumzie habari zilizo chini ya mojawapo ya vichwa vidogo katika ukurasa wa 16-17. Soma angalau andiko moja. Mtolee magazeti na upange kurudi ili mchunguze jibu la swali linalofuata. Ikiwa hamjapokea gazeti la Novemba 1 kutanikoni, toeni gazeti la karibuni zaidi na pendekezo la kutoa gazeti hilo linalopatikana katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Mnara wa Mlinzi Novemba 1
“Watu fulani huona kwamba maoni ya Biblia kuhusu ngono yamepitwa na wakati na yanawanyima uhuru. Wengine hukubaliana na Biblia. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho andiko hili linasema kuhusu chanzo cha viwango vya Biblia. [Soma 2 Timotheo 3:16.] Gazeti hili linaonyesha jinsi Biblia inavyojibu maswali kumi yanayoulizwa sana kuhusu ngono. Pia, linaeleza jinsi viwango vya Biblia vinavyotunufaisha.”
Amkeni! Novemba
“Unafikiri tunafikia mkataa gani tunapouchunguza ulimwengu kwa makini sana? Je, tunakata kauli kwamba kuna Muumba, au tunasema kwamba vitu vyote vilijitokeza vyenyewe tu? [Mruhusu ajibu.] Mwandishi mmoja wa Biblia alisema hivi baada ya kuuchunguza ulimwengu. [Soma Waroma 1:20.] Gazeti hili linaeleza mambo ambayo wanasayansi wamevumbua kuhusu chembe za mwanadamu na ambayo yanatusaidia kujua kama kuna Muumba au la.”