Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Novemba
“Ningependa kukuonyesha swali hili. [Soma swali la kwanza lililo kwenye ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1.] Una maoni gani? [Soma mafungu mawili yaliyo chini ya swali hilo na angalau andiko moja.] Je, naweza kukutembelea tena ili tuzungumzie kwa nini Yesu aliwafufua wafu na mambo ambayo tunajifunza?”
Manara wa Mlizi la Novemba 1
“Je, umewahi kujiuliza kwa nini mambo mengi mabaya hutukia duniani? [Mruhusu ajibu.] Biblia inaeleza sababu katika Ufunuo 12:9. [Soma.] Hata hivyo, mstari wa 12 unatoa tumaini. [Soma Ufunuo 12:12.] Uvutano mwovu wa Shetani utaondolewa hivi karibuni. Makala yenye kichwa ‘Je, Tunapaswa Kumwogopa Shetani?’ inazungumzia jinsi tunavyoweza kujilinda sasa kutokana na uvutano wa Shetani na kile kitakachompata Shetani hivi karibuni. Hii ni nakala yako.”
Amkeni la Novemba
“Kila mtu anataka kuwa na furaha, lakini watu wengi leo hawana furaha. Unafikiri ni nini kinachoongoza kwenye furaha ya kweli? [Mruhusu ajibu.] Biblia hutusaidia kuwa na maisha yenye furaha. Kwa mfano, fikiria kanuni hii ya Biblia. [Soma Waebrania 13:5.] Gazeti hili linazungumzia mambo manne yanayotegemea Biblia ambayo yanaongoza kwenye furaha ya kweli.”