Ratiba ya Juma Linaloanza Desemba 24
JUMA LINALOANZA DESEMBA 24
Wimbo 5 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 3 ¶1-6 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Zekaria 9-14 (Dak. 10)
Na. 1: Zekaria 11:1-13 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Mungu Husikiliza Sala za Nani?—rs uku. 257 ¶1–uku. 258 ¶3 (Dak. 5)
Na. 3: Ni Katika Hali Zipi Tunaweza Kutumia Kanuni Iliyo Katika Andiko la Methali 15:1? (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 30: Jinsi Tunavyoweza Kutumia Vizuri Tovuti Yetu Rasmi. Mazungumzo yanayotegemea ukurasa wa 3-6. Mnapozungumzia ukurasa wa 4, panga onyesho la dakika tatu la familia inayomalizia jioni yao ya Ibada ya Familia. Kichwa cha familia anaomba washiriki wa familia wapendekeze kile watakachojifunza juma linalofuata, na watoto wanaonyesha mambo ambayo wangependa kuzungumzia kwenye sehemu ya “Matineja” katika Tovuti. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wametumia au wanavyopanga kutumia Tovuti ya jw.org kwa ajili ya funzo la kibinafsi na la familia. Mnapozungumzia ukurasa wa 5, panga onyesho la dakika tatu la mhubiri mwenye kifaa kinachobebeka kilichounganishwa na Intaneti akitumia Tovuti yetu kumjibu mwenye nyumba swali linalohusu imani yetu. Mnapozungumzia ukurasa wa 6, panga onyesho la dakika nne la mhubiri anayezungumza na mtu anayependezwa, anayependelea kusoma katika lugha tofauti. Mhubiri anatumia kifaa chake kinachobebeka au kompyuta ya mwenye nyumba kumfungulia ukurasa kutoka katika trakti Kujua Ukweli au kitabu Biblia Inafundisha katika lugha ya mwenye nyumba, na kuizungumzia. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wametumia Tovuti ya jw.org kwenye huduma.
Wimbo 101 na Sala