Ratiba ya Juma Linaloanza Aprili 1
JUMA LINALOANZA APRILI 1
Wimbo 38 na Sala
□Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 7 ¶7-13 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Luka 7-9 (Dak. 10)
Na. 1: Luka 7:18-35 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Ni Taifa Gani Jipya Lililozaliwa Katika Pentekoste, na kwa Kusudi Gani?—Gal. 6:16; 1 Pet. 2:9 (Dak. 5)
Na. 3: Kaini Alipata Wapi Mke Wake?—rs uku. 95 ¶5–uku. 96 ¶1 [kwa habari zaidi ona w10 9/1 uku. 25](Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Njia za Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa Aprili. Mazungumzo. Tumia sekunde 30 hadi 60 ili kuonyesha kwa nini magazeti hayo yatawavutia watu katika eneo lenu. Kisha, kwa kutumia makala za kwanza za Mnara wa Mlinzi, waombe wasikilizaji wapendekeze swali linaloamsha upendezi ambalo watauliza, na kisha watoe mapendekezo ya andiko ambalo watasoma. Fanya vivyo hivyo kuhusu makala za kwanza za Amkeni! na, wakati ukiruhusu, kuhusu makala nyingine moja katika mojawapo ya magazeti hayo. Panga kuwe na onyesho la jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 10: Nufaika Kutokana na Kitabu cha Mwaka—2013. Mazungumzo. Zungumzia “Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza.” Panga mapema ili baadhi ya wahubiri wasimulie mambo yenye kutia moyo ambayo wamesoma kutoka kwenye Kitabu cha Mwaka. Waombe wasikilizaji waeleze mambo yenye kupendeza sana ya ripoti ya ulimwenguni pote. Malizia kwa kuwatia moyo wote wakamilishe usomaji wao wa Kitabu cha Mwaka.
Wimbo 75 na Sala