Matangazo
◼ Toleo la machapisho la mwezi wa Machi na Aprili: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu waliopendezwa, tumia kitabu Biblia Inafundisha au ikitegemea hali za yule unayezungumza naye, mojawapo ya broshua Msikilize Mungu au Msikilize Mungu Uishi Milele, na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Mei na Juni: Wahubiri wanaweza kutoa mojawapo ya trakti zifuatazo: Je!, Ulimwengu Huu Utaokoka?, Je, Una Roho Isiyoweza Kufa?, Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa?, Kuteseka Kote Kutaisha Karibuni!, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?, Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani, au Yehova—Yeye Ni Nani? Ikiwa mtu amependezwa kwelikweli, onyesha jinsi funzo la Biblia linavyofanywa ukitumia kitabu Biblia Inafundisha au mojawapo ya broshua Msikilize Mungu au Msikilize Mungu Uishi Milele.
◼ Ukumbusho utaadhimishwa, Jumanne, Machi 26, 2013. Ikiwa kutaniko lenu hufanya mkutano siku ya Jumanne, mnapaswa kufanya mkutano huo siku nyingine katika juma hilo ikiwa Jumba la Ufalme halitakuwa likitumiwa. Iwapo Jumba lenu la Ufalme linatumiwa na makutaniko kadhaa na haiwezekani kufanya mikutano siku nyingine, mratibu wa baraza la wazee anaweza kupanga ili sehemu ambazo hasa zinahusu kutaniko lenu, zizungumziwe katika Mkutano mwingine wa Utumishi mwezi huo. Makutaniko yanayotembelewa na mwangalizi wa mzunguko yanapaswa kufanya mipango ili mikutano ambayo hufanywa Jumanne jioni ifanywe jioni nyingine wakati wa ziara.