Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/13 uku. 8
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 3/13 uku. 8

Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Aprili

“Tunawatia moyo jirani zetu wasome Biblia zao. Lakini watu wengi huhisi ni vigumu kuelewa Biblia. Je, wewe umeona hivyo? [Mruhusu ajibu.] Ona jambo hili.” Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, na mzungumzie pamoja habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mwachie magazeti na ufanye mipango ya kurudi ili mzungumzie swali linalofuata. Tumia magazeti ya karibuni zaidi mliyo nayo kutanikoni yaliyo na mapendekezo ya jinsi ya kuyatoa kutoka kwenye Huduma ya Ufalme iliyo na mapendekezo hayo.

Mnara wa Mlinzi Aprili 1

“Kila mtu tunayezungumza naye hukabiliana na matatizo fulani. Hilo hufanya baadhi ya watu wajiulize ni nini kusudi la uhai. Unafikiri ni jambo gani kubwa linalowazuia watu kuwa na furaha leo? [Mruhusu ajibu.] Biblia inaahidi kwamba hivi karibuni Mungu ataondoa matatizo tunayokabili leo. [Soma Ufunuo 21:4.] Gazeti hili linazungumzia mambo tunayotazamia wakati ujao na vilevile jinsi tunavyoweza kupata kusudi la maisha hata sasa.”

Amkeni! Aprili

“Jeuri inayotendeka nyumbani ni tatizo la ulimwenguni pote. Wengine husema kwamba mambo yanayochangia tatizo hilo ni utamaduni wa mtu mwenyewe, malezi yake, na burudani zenye jeuri. Unafikiri ni nini hasa kinachosababisha jeuri nyumbani? [Mruhusu ajibu.] Biblia inaonyesha uhusiano unaofaa unaopaswa kuwa kati ya mume na mke. [Soma Waefeso 5:33.] Gazeti hili linazungumzia jinsi baadhi ya ndoa zilivyoweza kuokolewa kwa kutumia kanuni za Biblia.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki