Ratiba ya Juma Linaloanza Aprili 15
JUMA LINALOANZA APRILI 15
Wimbo 6 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 8 ¶1-7 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Luka 13-17 (Dak. 10)
Na. 1: Luka 16:16-31 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Je, Hali Yetu ya Kutokamilika Inamaanisha Kwamba Sisi Hatuna Thamani Machoni pa Mungu?—Zab. 103:8, 9, 14; Gal. 6:9 (Dak. 5)
Na. 3: Je, Wanadamu Wote Ni Watoto wa Mungu?—rs uku. 98 ¶1–5 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Sanduku la Swali. Mazungumzo.
Dak. 10: Njia za Kupanua Huduma Yako—Sehemu ya 2. Hotuba inayotegemea kitabu Tengenezo, ukurasa wa 112, fungu la 3, hadi ukurasa wa 114, fungu la 1. Mhoji painia mmoja au wawili kuhusu jinsi walivyoweza kufanya marekebisho ili waweze kufanya upainia.
Dak. 10: Je, Wewe Hutoa Ushahidi Kazini? Mazungumzo yanayotegemea maswali yafuatayo. (1) Kwa nini ni vizuri wafanyakazi wenzako wajue kwamba wewe ni Shahidi wa Yehova? (2) Unawezaje kuwajulisha? (3) Ni hali gani zinazoweza kukupa nafasi ya kutoa ushahidi ukiwa kazini? (4) Ikiwa inawezekana, kwa nini ni vizuri kuweka Biblia na machapisho kadhaa mahali unapofanyia kazi? (5) Kwa nini ni vizuri kuepuka kutumia muda mrefu kupita kiasi kutoa ushahidi wakati wa kazi? (6) Umejionea mambo gani mazuri kwa kutoa ushahidi kazini?
Wimbo 45 na Sala