Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Katika mwezi wa Desemba, wahubiri 172 walibatizwa.
Sudan: Lilikuwa jambo lenye kutia moyo sana kwa kuwa mafunzo ya Biblia 920 yaliongozwa nchini Sudan katika mwezi wa Desemba! Jumla ya watu 927 walihudhuria makusanyiko ya wilaya ya mwaka wa 2012 na watu 6 walibatizwa.
Sudan Kusini: Mwezi wa Desemba ulikuwa mwezi mzuri wa utumishi wa shambani nchini Sudan Kusini, kwani kulikuwa na vilele vipya vya wahubiri na ziara za kurudia. Kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 1,274. Hilo ni ongezeko la asilimia 16 ikilinganishwa na wastani wa mwaka uliopita. Jumla ya watu 3,961 walihudhuria makusanyiko ya wilaya ya mwaka wa 2012 na watu 46 walibatizwa.