Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/13 uku. 8
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Mapendekezo Kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 6/13 uku. 8

Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Julai

“Karibu kila mtu katika eneo letu angependa kuishi maisha marefu, yenye furaha. Kwa hiyo tungependa kujua maoni yako kuhusu swali hili: Je, unafikiri kwamba siku moja maendeleo ya kisayansi na kitiba yataweza kutusaidia kuishi milele? [Mruhusu ajibu.] Ona jambo hili.” Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, na mzungumzie habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mwachie magazeti, na ufanye mipango ya kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.

Zingatia: Kwa kutumia pendekezo lililo hapo juu, fanyeni mpango kuwe na onyesho litakalofanywa tarehe 6 mwezi wa Julai wakati wa mkutano wa utumishi wa shambani.

Mnara wa Mlinzi Julai 1

“Watu wengi tunaozungumza nao wana dini zao. Lakini wengine wanasema kwamba hawana imani kabisa katika dini. Una maoni gani kuhusu dini? [Mruhusu ajibu.] Yesu aliweka kiwango cha kutusaidia kuchunguza dini. [Soma Luka 6:44a.] Gazeti hili linazungumzia baadhi ya matunda mabaya ambayo yametokezwa na dini. Pia linajibu swali hili: Je, kuna dini inayoweza kutegemeka?”

Amkeni! Julai

“Tunawatembelea majirani wetu ili kuzungumzia tatizo la ukosefu wa haki linalowahangaisha watu sana. Kuna watu ambao hupinga ukosefu wa haki kwa kufanya maandamano. Je, unafikiri kwamba watu wanaofanya hivyo hufanikiwa kuleta mabadiliko? [Mruhusu ajibu.] Biblia inaonyesha jambo litakaloleta mabadiliko ya kudumu duniani. [Soma Mathayo 6:9, 10.] Gazeti hili linajibu swali hili: Je, Maandamano Ndilo Suluhisho la Matatizo ya Ulimwengu?”

Habari Njema Kutoka kwa Mungu!

“Tunawatembelea ili kushiriki pamoja nanyi jambo lenye kutia moyo kutoka katika Biblia. Wengi ambao tumezungumza nao hawaelewi kwa nini Mungu mwenye upendo anaweza kuruhusu watu wateseke sana ulimwenguni. Je, unafikiri kuteseka kulikuwa sehemu ya kusudi la awali la Mungu kwa dunia?” Mruhusu ajibu. Kisha fungua Somo la 5, na usome na kuzungumzia mafungu mawili ya kwanza na maandiko yaliyo katika herufi za mlazo. Mwachie broshua hiyo, na ufanye mipango ya kurudi ili mzungumzie swali linalofuata lililoandikwa kwa maandishi yenye wino mzito.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki