Ratiba ya Juma Linaloanza Agosti 5
JUMA LINALOANZA AGOSTI 5
Wimbo 77 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 12 ¶20-25, sanduku kwenye uku. 151 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Waroma 1-4 (Dak. 10)
Na. 1: Waroma 3:21–4:8 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Kwa Nini Wakristo Hujiona Kama “Wageni na Wakaaji wa Muda” Ulimwenguni?—1 Pet. 2:11; 1 Yoh. 2:15-17 (Dak. 5)
Na. 3: Wakristo wa Kweli Watapata Ulinzi Gani Wakati wa Dhiki Kuu?—rs uku. 114 ¶1-5 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Njia za Kutoa Magazeti ya Karibuni Zaidi Katika Mwezi wa Agosti. Mazungumzo. Tumia sekunde 30 hadi 60 kueleza kwa nini magazeti hayo yatawavutia watu katika eneo lenu. Halafu, kwa kutumia habari kuu ya gazeti la Mnara wa Mlinzi, waombe wasikilizaji wapendekeze swali linaloamsha upendezi ambalo watauliza na kisha watoe mapendekezo ya andiko ambalo watasoma. Fanya vivyo hivyo kuhusu gazeti la Amkeni! na wakati ukiruhusu, kuhusu makala nyingine moja kutoka katika mojawapo ya magazeti hayo. Panga kuwe na onyesho la jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 10: Tunajifunza Nini? Mazungumzo. Waombe wasikilizaji wasome Luka 5:27-32. Zungumzia jinsi masimulizi hayo yanavyoweza kutusaidia katika huduma yetu.
Wimbo 119 na Sala