Ratiba ya Juma Linaloanza Desemba 9
JUMA LINALOANZA DESEMBA 9
Wimbo 84 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jl Somo la 17-19 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Yohana 1–Yuda (Dak. 10)
Na. 1: 1 Yohana 5:1-21 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Yesu Kristo Anapaswa Kukumbukwaje?—Luka 1:32, 33; Yohana 17:3 (Dak. 5)
Na. 3: Dini ya Kweli Huonyesha Imani ya Kweli Katika Yesu Kristo—rs uku. 65 ¶3 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 15: Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2014. Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Ukitumia maagizo ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2014, zungumzia mambo ambayo kutaniko lenu linahitaji kuzingatia. Eleza kwamba ikiwa usomaji wa Biblia utakuwa ukizungumzia sura za kwanza za kitabu, hakuna haja ya kuzumgumzia mambo makuu katika kitabu “Kila Andiko”. Ikiwa chanzo cha habari za hotuba Na. 2 na Na. 3 ni kitabu Kutoa Sababu, au Vichwa vya Mazungumzo ya Biblia [td] mafungu yanayorejelewa ni yale tu ambayo yanaanza kwa sentensi iliyoingizwa ndani kidogo. Watie moyo wote watimize migawo yao kwa bidii, watoe maelezo wakati wa mambo makuu ya usomaji wa Biblia, na watumie mapendekezo yanayotolewa kila juma katika kitabu Shule ya Huduma.
Dak. 15: “Jinsi ya Kutayarisha Utangulizi Wenye Matokeo.” Maswali na majibu. Panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa kitabu Biblia Inafundisha, la kwanza liwe na utangulizi usio na matokeo, la pili liwe na utangulizi wenye matokeo.
Wimbo 60 na Sala