Ratiba ya Juma Linaloanza Desemba 16
JUMA LINALOANZA DESEMBA 16
Wimbo 116 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jl Somo la 20-22 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Ufunuo 1-6 (Dak. 10)
Na. 1: Ufunuo 3:14–4:8 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Dini ya Kweli Si ya Kidesturi, Bali Ni Njia ya Maisha Yetu—rs uku. 65 ¶4 (Dak. 5)
Na. 3: Ni Katika Njia Zipi Yesu ‘Aliweka Kielelezo’ kwa Ajili ya Wanafunzi Wake?—Yohana 13:15 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Tulitimiza Nini? Mazungumzo yatakayofanywa na mwangalizi wa utumishi. Waeleze wahubiri ni eneo kubwa kadiri gani lililohubiriwa wakati wa kampeni ya trakti Habari za Ufalme Na. 38. Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi walivyonufaika kwa kushiriki katika kampeni hiyo na watoe maelezo kuhusu mambo yoyote yenye kuvutia.
Dak. 10: Vijana Msifuni Yehova. (Zab. 148:12, 13) Mhoji kijana mmoja ambaye ni mfano mzuri. Anakabili hali gani ngumu kuhusiana na imani yake? Wazazi na wengine wamemsaidiaje kukabiliana na hali hiyo? Amepata wapi ujasiri wa kutoa ushahidi kuhusu imani yake? Malizia kwa kuwatia moyo vijana wajitayarishe kwa ajili ya mwaka mpya wa shule na utaje baadhi ya changamoto ambazo huenda wakakabili.
Dak. 10: “Tutaanza Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova Juma Linaloanza Januari 6.” Maswali na majibu.
Wimbo 75 na Sala