Matangazo
◼ Machapisho yatakayotolewa mwezi wa Februari: Habari Njema Kutoka kwa Mungu! au mojawapo ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je, Kweli Mungu Anatujali?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!, Lasting Peace and Happiness—How to Find Them, au Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? Unapofanya ziara za kurudia, tumia kitabu Biblia Inafundisha au ikitegemea hali za yule unayezungumza naye, mojawapo ya broshua, Msikilize Mungu au Msikilize Mungu Uishi Milele, na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Machi na Aprili: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mei na Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? au mojawapo ya trakti zifuatazo: Kuteseka Kote Kutaisha Karibuni!, Yehova—Yeye Ni Nani?, Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani, au Je, Ungependa Kujua Ukweli?
◼ Kichwa cha hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho wa 2014 kitakuwa “Kwa Nini Mungu Mwenye Upendo Ameruhusu Uovu?”
◼Wahubiri wanaposhiriki katika mahubiri ya hadharani kwa kutumia meza au kigari cha kukokotwa, hawapaswi kuweka Biblia mahali zinapoonekana. Hata hivyo, wanaweza kuwa na Biblia za kuwapa watu wanaoziulizia au wanaopendezwa kwelikweli.