Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/14 uku. 4
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 2/14 uku. 4

Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Machi

“Tunawatembelea kifupi kwa sababu ya tukio litakalofanywa mwezi wa Aprili tarehe 14. Tarehe hiyo ni ukumbusho wa kifo cha Yesu. Wengine wataadhimisha ukumbusho kwa sababu wanafikiri kwamba kifo chake ni muhimu. Ilhali wengine hawana uhakika ikiwa kifo cha Yesu ni muhimu. Je, unafikiri kwamba kifo cha Yesu kina faida kwetu?” Mruhusu ajibu. Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 1, na mzungumzie pamoja habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau andiko moja lililoonyeshwa. Mwachie magazeti, na ufanye mpango wa kuzungumzia swali linalofuata.

Mnara wa Mlinzi Machi 1

“Watu wengi hujiuliza ni kwa nini Mungu haingilii kati ili kukomesha ukosefu wa haki na kuteseka ulimwenguni. Je, unafikiri ni kwa sababu Mungu hajali au anaona ni vizuri wanadamu wateseke? [Mruhusu ajibu. Halafu soma Yohana 3:​16.] Ingawa wengi hunukuu mstari huu kuonyesha kwamba Mungu anajali, hawana uhakika ni katika njia gani wananufaika kutokana na kifo cha mwana wa Mungu. Gazeti hili linaeleza jinsi kifo cha Yesu kinavyofanya iwezekane kukomeshwa kwa ukosefu wa haki na kuteseka ulimwenguni.”

Amkeni Machi

“Tumekutembelea kifupi ili kurekebisha maoni yasiyofaa kuhusu mstari huu wa Biblia. [Soma Mwanzo 1:1.] Baadhi ya watu huamini jambo hili kwamba ulimwengu uliumbwa, ilhali wengine hawaamini. Labda nikuulize, je, wewe una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi wanashindwa kuamini uumbaji kwa sababu viongozi wa dini hawafundishi yale ambayo Biblia inasema. Gazeti hili linaonyesha jinsi Biblia inavyoeleza hatua kwa hatua uthibitisho usioweza kupingwa kuhusu mwanzo wa ulimwengu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki