Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kwa Ajili ya Kampeni ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho
“Tunawapa watu mwaliko huu wa kuhudhuria tukio muhimu sana. Tarehe 3 mwezi wa Aprili, mamilioni ya watu ulimwenguni pote watakusanyika ili kukumbuka kifo cha Yesu Kristo na pia kusikiliza bila malipo hotuba itakayotolewa ambayo itazungumzia jinsi tunavyofaidika kutokana na kifo cha Yesu. Mwaliko huu unaonyesha wakati na mahali pa mkutano.”
Mnara wa Mlinzi Machi 1
“Ukumbusho wa kifo cha Yesu Kristo utakuwa tarehe 3 mwezi wa Aprili. Baadhi ya watu katika eneo letu watakutana ili kukumbuka tukio hilo, lakini kuna watu fulani ambao wanafikiri kwamba kifo cha Yesu hakikuwa na maana yoyote. Una maoni gani? Je, unafikiri kwamba kifo cha Yesu na ufufuo wake una faida kwetu? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi Neno la Mungu linavyosema kuhusu jambo hilo. [Soma 1 Wakorintho 15:22, 26.] Gazeti hili linazungumzia baraka tutakayopata wakati ujao kutokana na dhabihu ya fidia ya Yesu, yaani, kuondolewa kwa kifo duniani.”
Amkeni Machi
“Tumewatembelea kwa ufupi ili kuwaonyesha gazeti hili la Amkeni! [Onyesha jalada la gazeti hilo.] Watu wana maoni tofauti kuhusu swali hili: ‘Je, kuna Mungu?’ Kati ya watu wanaomwamini Mungu na wale wasiomwamini, unafikiri ni nani walio na mtazamo mzuri zaidi kuhusu wakati ujao? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi hii kutoka kwa Mungu inayowapa watu wengi tumaini. [Soma Zaburi 37:10, 11.] Gazeti hili linaonyesha sababu nne zinazothibitisha kwamba kuna Mungu.”