Ratiba ya Juma Linaloanza Aprili 7
JUMA LINALOANZA APRILI 7
Wimbo 15 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 5 ¶9-17 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Kutoka 7-10 (Dak. 10)
Na. 1: Kutoka 9:20-35 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Yesu Atakuja Katika Hali Gani, na Kila Jicho Litamwona Jinsi Gani?—rs uku. 117 ¶4 –uku. 118 ¶5 (Dak. 5)
Na. 3: Biblia Inasema Nini Kuhusu Ukumbusho wa Mlo wa Jioni wa Bwana?—td 36A (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Toa Magazeti Mwezi wa Aprili. Mazungumzo. Anza kwa onyesho la jinsi ya kutoa magazeti, tumia mapendekezo mawili yaliyo kwenye ukurasa huu. Halafu chunguza mapendekezo hayo kuanzia mwanzo hadi mwisho. Malizia kwa kuwatia moyo wote wasome magazeti vizuri na wayatoe kwa shauku.
Dak. 10: Msisahau Ukaribishaji-Wageni. (Ebr. 13:1, 2) Hotuba itolewe na mzee. Taja mipango ya kutaniko kwa ajili ya Ukumbusho. Toa mapendekezo ya jinsi kila mhubiri anavyoweza kuwakaribisha wageni na wahubiri wasiotenda watakaohudhuria Ukumbusho. Panga kuwe na onyesho fupi lenye sehemu mbili. Katika sehemu ya kwanza ya onyesho, kabla tu Ukumbusho haujaanza, mhubiri anamkaribisha mtu aliyepata mwaliko. Na katika sehemu ya pili ya onyesho, baada ya Ukumbusho, mhubiri anafanya mipango ya kukutana na mtu huyo tena.
Dak. 10:Tulitimiza Nini? Mazungumzo. Waombe wahubiri waeleze jinsi walivyonufaika kwa kutumia madokezo yaliyo kwenye makala “Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Jinsi ya Kumjibu Mtu Anayekataa Mazungumzo,” Waombe wasikilizaji waeleze mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo.
Wimbo 20 na Sala