Matangazo
Machapisho yatakayotolewa mwezi wa Machi na Aprili: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mei na Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? au mojawapo ya trakti zifuatazo: Je, Ungependa Kujua Ukweli?, Kuteseka Kote Kutaisha Karibuni!, Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani, au Yehova—Yeye Ni Nani? na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Ukumbusho utaadhimishwa Jumatatu, Aprili 14, 2014. Ikiwa kutaniko lenu kwa kawaida linafanya mikutano Jumatatu, inapaswa kubadilishwa na kufanywa siku nyingine katika juma hilo iwapo nafasi itapatikana. Ikiwa haitawezekana kufanya Mkutano wa Utumishi, mratibu wa baraza la wazee anaweza kufanya marekebisho katika ratiba ili hasa sehemu zinazohusu kutaniko lenu zizungumziwe mwezi huohuo.
Kichwa cha hotuba ya watu wote itakayotolewa na mwangalizi wa mzunguko katika nusu ya pili ya mwaka wa utumishi ni “Kukombolewa Kutoka Kwenye Ulimwengu Wenye Taabu.”