Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kwa Ajili ya Kampeni ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho
“Tunatoa mialiko kwa ajili ya tukio muhimu sana. Tarehe 14 mwezi wa Aprili, mamilioni ya watu duniani pote watakusanyika ili kuadhimisha kifo cha Yesu na kusikiliza hotuba ya Biblia itakayozungumzia manufaa tunayopata kutokana na kifo chake. Mwaliko huu unaonyesha mahali na wakati ambao mkutano huo utafanyika katika eneo letu.”
Mnara wa Mlinzi Aprili 1
“Tumewatembelea ili kuzungumzia jambo fulani ambalo watu wengi hufanya. Karibu kila mtu husali haidhuru ni wa dini gani. Je, unafikiri Mungu hujibu sala, au tunasali ili tu tuhisi tumepata kitulizo kutokana na matatizo yetu? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi Biblia inavyosema kuhusu sala. [Soma 1 Yohana 5:14.] Gazeti hili linaelezea manufaa tunayopata tunaposali.”
Amkeni Aprili
“Tumewatembelea ili kuwapa msaada wa tatizo ambalo linawahangaisha watu wengi. Watu wengine huhisi wamelemewa sana na matatizo hivi kwamba wanafikiria kujiua. Ikiwa mtu anahisi hivyo, je, unafikiri kwa kweli anataka kufa, au anataka tu kupata kitulizo? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi ya Biblia ambayo imewasaidia wengi kudumisha mtazamo unaofaa. [Soma Ufunuo 21:3, 4.] Gazeti hili linazungumzia sababu tatu za kuendelea kuishi licha ya matatizo ambayo watu hukabili.”