Habari Kuu za Utumishi
Sudan: Idadi ya mafunzo ya Biblia yaliyoongozwa ilikuwa ya pekee sana, kwani wahubiri waliongoza mafunzo ya Biblia 995 na kufanya ziara za kurudia 7,336.
Sudan Kusini: Katika mwezi wa Januari wahubiri walifurahia sana utumishi wa shambani licha ya magumu waliyokabili. Waliongoza mafunzo ya Biblia 2,672 na kufanya ziara za kurudia 19,930.
Uganda: Ripoti ya utumishi wa shambani ya mwezi wa Januari ilikuwa yenye kutia moyo sana. Kulikuwa na vilele vipya vya wahubiri 6,420, mapainia 835, ziara za kurudia 97,633, na mafunzo ya Biblia 18,456.