Ratiba ya Juma Linaloanza Agosti 11
JUMA LINALOANZA AGOSTI 11
Wimbo 71 na Sala
cl sura ya 11 ¶9-16 (Dak. 30)
Usomaji wa Biblia: Hesabu 7-9 (Dak. 10)
Na. 1: Hesabu 9:9-23 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Mtu Akiokolewa Haimaanishi Kwamba Ameokolewa Siku Zote—rs uku. 417 ¶1–4 (Dak. 5)
Na. 3: Uponyaji wa Imani wa Sasa Hauna Uthibitisho wa Kibali cha Mungu—td 16C (Dak. 5)
Dak. 5: “1914-2014 Miaka Mia Moja ya Utawala wa Ufalme!” Mazungumzo. Omba msikilizaji mmoja asome fungu lililo juu katika ukurasa huu. Sehemu za Mkutano wa Utumishi mwezi huu zitakazia Ufalme. Taja mipango ya utumishi ya kutaniko lenu.
Dak. 10: “Tumia Trakti Mpya ya Tovuti.” Zungumzia yaliyomo kwenye trakti. Panga kuwe na onyesho la mhubiri anayetoa trakti, na kisha anatumia kifaa chake cha kielektroniki kumwelekeza mtu kwenye Tovuti ya jw.org. Katika eneo ambalo trakti hiyo haitafaa, tumia trakti, Je, Ungependa Kujua Ukweli? Muulize mwenye nyumba ni swali gani linalompendeza zaidi, na uzungumzie kwa ufupi jibu la swali hilo kulingana na Biblia, kisha weka msingi wa kufanya ziara ya kurudia.
Dak. 15: “Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Zungumza kwa Ujasiri Kuhusu Ufalme.” Mazungumzo. Panga wahubiri wawili wafanye onyesho lifuatalo: Mhubiri yuko kwenye foleni dukani. Mtu aliyesimama kando yake anasoma gazeti na kusema: “Ulimwengu huu umeharibika! Kila mtu anajifanya anajua, lakini mambo yanazidi kuwa mabaya.” Mhubiri anajizungumzia: ‘Napaswa kusema jambo fulani. Napaswa kumweleza kuhusu Ufalme!’ Mhubiri anasema: “Ni kweli, kuna habari nyingi mbaya. Lakini ningependa kukupatia trakti hii. Inazungumzia Tovuti ambayo imenisaidia kupata majibu ya maswali mengi muhimu maishani.” Mhubiri anamwonyesha jambo moja lililo kwenye trakti, na mtu huyo anaonyesha upendezi.
Wimbo 92 na Sala