Matangazo
◼ Toleo la machapisho la mwezi wa Septemba na Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Novemba na Desemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? au mojawapo ya trakti zifuatazo: Je, Kuteseka Kutaisha?, Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?, Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?, au Ni Nini Siri ya Kuwa na Familia Yenye Furaha?
◼ Hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho katika mwaka wa 2015 itatolewa juma la Aprili 6. Kichwa cha hotuba hiyo kitatangazwa baadaye. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko mwishoni mwa juma hilo, yatakuwa na hotuba ya pekee juma litakalofuata. Hotuba hiyo haipaswi kutolewa katika kutaniko lolote kabla ya Aprili 6.
◼ Kuanzia Septemba, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Jinsi Hekima ya Mungu Inavyotunufaisha.”