Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Oktoba
“Tunawatembelea jirani zetu kwa muda mfupi ili kuzungumzia kuhusu serikali bora. Je, unafikiri kuna serikali yoyote inayoweza kuondoa matatizo sugu, kama vile uhalifu na ukosefu wa haki?” Mruhusu ajibu. Mkumbushe mwenye nyumba kwamba katika Sala ya Bwana, Yesu aliwafundisha wanafunzi wake waombe serikali ya aina hiyo, yaani, Ufalme wa Mungu, uje. Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, na mzungumzie pamoja habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau andiko moja lililoonyeshwa. Mwachie magazeti na ufanye mpango wa kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Oktoba 1
“Tunazungumza kwa ufupi na jirani zetu kuhusu maneno haya yanayopatikana katika sala ambayo Yesu aliwafundisha wafuasi wake. [Soma Mathayo 6:9, 10.] Je, unafahamu Ufalme wa Mungu ni nini, na kwa nini Yesu aliuzungumzia sana katika mafundisho yake? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha mambo ambayo Biblia inasema kuhusu Ufalme wa Mungu na baraka utakazoleta duniani.”
Amkeni Oktoba
“Tunawatembelea watu kwa muda mfupi ili kuwasaidia kupata jibu la swali hili. [Mwonyeshe jalada la gazeti.] Je, unafikiri kwamba ili kupata mafanikio ya kweli ni lazima mtu awe tajiri? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatusaidia kuwa na maoni yanayofaa kuhusu mali. [Soma Luka 12:15.] Biblia inaonyesha kwamba mtu yeyote anaweza kupata mafanikio ya kweli. Gazeti hili linafafanua jambo hilo.”