Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Oktoba
“Katika nyakati hizi ngumu, sote tunakabili matatizo yanayosababisha mikazo katika familia. Unafikiri tunaweza kupata wapi mwongozo wenye kutegemeka utakaotusaidia kufanya maisha ya familia yetu yawe yenye furaha?” Mruhusu ajibu. Kisha umpe mwenye nyumba nakala ya Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, na mzungumzie pamoja habari zilizo chini ya mojawapo ya vichwa vidogo kwenye ukurasa wa 16 na 17 na angalau moja ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mtolee magazeti, na upange kurudi ili mzungumzie mojawapo ya maswali hayo mengine.
Mnara wa Mlinzi Oktoba 1
Mwonyeshe gazeti na umuulize, “Ungehisije ukijua kwamba ulikuwa umeambiwa habari za uwongo kumhusu Mungu? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Yesu alisema kuhusu jinsi tunavyoweza kutofautisha ukweli kutoka kwa uwongo. [Soma Yohana 17:17.] Hivyo, ni Biblia pekee inayotuambia ukweli kumhusu Mungu. Gazeti hili linazungumzia mafundisho matano ya uwongo kumhusu Mungu, ambayo Biblia inafunua.”
Amkeni! Oktoba
“Leo tunawatembelea watu wote tukiwa na ujumbe kwa ajili ya familia. Unafikiri wazazi wanakabili tatizo gani kubwa leo wanapowalea watoto wao? [Mruhusu ajibu.] Wazazi wengi hutegemea Biblia ili kupata ushauri. Kwa mfano, maneno haya ya hekima yanaweza kukusaidia unapowatia watoto nidhamu. [Soma Waefeso 4:31.] Gazeti hili linaonyesha jinsi ushauri wa Biblia unavyoweza kuwasaidia wazazi katika kila hatua ya ukuzi wa watoto wao, tangu utotoni hadi ujanani.”