Mapendekezo Kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Oktoba
“Nina hakika utakubali kwamba maisha ni mafupi sana. Je, unafikiri siku moja tutaweza kuondoa magonjwa na kurefusha maisha yetu? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho gazeti hili linasema.” Mpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, na mzungumzie habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 na andiko lililoonyeshwa. Mwachie magazeti na ufanye mipango ya kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Oktoba 1
“Tunawatembelea kwa sababu wengi huhangaikia ufisadi uliopo katika biashara na serikali. Je, unafikiri kunaweza kuwa na suluhisho lolote? [Mruhusu ajibu.] Ona andiko hili linavyosema kuhusu jinsi Yesu atakavyowatendea walioathiriwa na ufisadi. [Soma Zaburi 72:12-14.] Gazeti hili linaonyesha jinsi ufisadi utakavyokomeshwa hivi karibuni.”
Amkeni! Oktoba
“Wazazi wengi wangependa watoto wao wapate elimu nzuri. Je, unafikiri vijana wanaohitimu shule siku hizi wako tayari kukabiliana na matatizo ya maisha? [Mruhusu ajibu.] Ona yale ambao Biblia husema kuhusu umuhimu wa kupata ujuzi na hekima. [Soma Mhubiri 7:12.] Gazeti hili linatoa mapendekezo matano yanayofaa ili kuwasaidia watoto wafaulu shuleni.”