Kwa Nini Tuondoke Bila Kukawia?
Ni kawaida kuwa na mazungumzo na ndugu zetu tunapokutana kwa ajili ya utumishi wa shambani. Hata hivyo, baada ya mkutano wa utumishi, tunapaswa kuondoka bila kukawia. Kazi yetu ya kuhubiri ni ya uharaka. (2 Tim. 4:2) Kadiri tunavyozidi kukawia, ndivyo tutakavyokuwa na muda mchache zaidi kwa ajili ya utumishi. Tutakuwa na nafasi nyingi za kufurahia ushirika wenye kujenga pamoja na wahubiri wenzetu tunapohubiri nao. Tunapoondoka bila kukawia ili kushiriki katika huduma, tunaonyesha kwamba sisi si wavivu tunapomtumikia Yehova na Mwana wake.—Rom. 12:11.