Ratiba ya Juma Linaloanza Februari 16
JUMA LINALOANZA FEBRUARI 16
Wimbo 80 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 20 ¶8-15 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Waamuzi 15-18 (Dak. 8)
Na. 1: Waamuzi 16:13-24 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Biblia Ina Ujumbe Gani?—igw uku. 8 ¶1-4 (Dak. 5)
Na. 3: Misa si ya Kimaandiko—td 36B (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: Uwe na “Bidii kwa Ajili ya Kazi Njema”!—Tito 2:14.
Dak. 15: Jitayarishe Kutangaza Habari Njema kwa Bidii. Mazungumzo. Tunapojitayarisha kwa ajili ya huduma kwa nini ni muhimu kusali kwanza kwa Yehova? (Zab. 143:10; Mdo. 4:31) Ni nini kingine tunachopaswa kufanya? (Ezra 7:10) Tunawezaje kupanga machapisho na mikoba yetu ya utumishi? Matayarisho mazuri yatatusaidiaje? (Ona gazeti la Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 2008, uku. 9, fu. 9.) Unajitayarishaje kwa ajili ya huduma? Panga kuwe na onyesho la mhubiri anayejitayarisha kwa ajili ya huduma kwa kupitia trakti, magazeti, na broshua ambazo atatumia. Kisha anapanga mkoba wake wa utumishi na kuhakikisha kwamba kifaa chake cha kielektroniki kinafanya kazi vizuri. Kazia kwamba sote tunapaswa kujitayarisha vizuri ili kushiriki katika huduma. (2 Tim. 3:17)
Dak. 15: “Je, Utaiga Bidii ya Yehova na Yesu Katika Majira Haya ya Ukumbusho?” Maswali na majibu. Mpe kila aliyehudhuria mwaliko wa Ukumbusho, na uzungumzie yaliyomo. Panga kuwe na onyesho fupi linalotegemea pendekezo lililo kwenye ukurasa wa 4.
Wimbo 30 na Sala