Kuchocheana kwa Bidii Katika Matendo Mazuri
Andiko la Waebrania 10:24 linatutia moyo “tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri.” Tunaweza kuwachochea ndugu zetu kupitia imani yetu na mfano tunaowawekea. Waeleze wengine kutanikoni mambo yenye kutia moyo uliyojionea. Acha waone shangwe unayopata kwa kumtumikia Yehova. Lakini epuka kuwalinganisha na wengine au kulinganisha hali zao na zako. (Gal. 6:4) Tunapaswa kutumia uwezo wetu kuwachochea wengine katika “upendo na matendo mazuri,” wala si katika hatia na matendo mazuri. (Ona kitabu Shule ya Huduma, uku. 158, fu. 3.) Tukiwachochea katika upendo, basi watatenda matendo mazuri kama vile kuonyesha ukarimu au kuhubiri.—2 Kor. 1:24.