Ratiba ya Juma Linaloanza Mei 18
JUMA LINALOANZA MEI 18
Wimbo 50 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 24 ¶18-21, sanduku kwenye uku. 249 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 9-12 (Dak. 8)
Na. 1: 2 Samweli 10:13–11:4 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Jinsi ya Kuitambua Dini ya Kweli —td 4A (Dak. 5)
Na. 3: Kuna Tumaini Gani kwa Ajili ya Wafu?—igw uku. 19 ¶1-3 (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: Wasaidie watu wa namna zote wapate ujuzi sahihi wa kweli.—1 Tim. 2:3, 4.
Dak. 10: Jinsi Paulo Alivyowasaidia Wagiriki Kupata Ujuzi Sahihi wa Kweli. Mazungumzo. Waombe wasikilizaji wasome Matendo 17:22-31. Zungumzia jinsi simulizi hilo linavyoweza kutusaidia katika huduma.
Dak. 20: Yehova Atakusaidia Uwe Jasiri. Mazungumzo. Onyesha video Yehova Atakusaidia Uwe Jasiri. (Tembelea jw.org/sw, na utafute chini ya MAFUNDISHO YA BIBLIA > WATOTO.) Waombe wasikilizaji waeleze mambo waliyojifunza kutokana na video hiyo. Waombe watoto wanaoenda shule waeleze jinsi video hiyo ilivyowasaidia kuwa na ujasiri wa kuwahubiria wanafunzi wenzao na walimu. Panga kuwe na onyesho la jinsi mwanafunzi alivyopata matokeo mazuri alipotoa ushahidi shuleni. Ikiwa video hizo hazipatikani, panga mapema kuwahoji wanafunzi kadhaa ambao wamekuwa wakitoa ushahidi shuleni. Walipataje ujasiri wa kutoa ushahidi shuleni? Eleza kwamba sala iliwasaidia Wakristo wa karne ya kwanza kusema Neno la Mungu kwa ujasiri.—Mdo. 4:31; ona gazeti la Mnara wa Mlinzi, la Februari 15, 2010, ukurasa wa 6, fungu la 7 na Februari 15, 2015, ukurasa wa 12, fungu la 7-9.
Wimbo 60 na Sala