Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Agosti 31, 2015.
Ni kweli gani zenye kujenga imani kumhusu Yehova Mungu tunazopata katika sala ya Sulemani, na kutafakari kweli hizo kutatunufaishaje? (1 Fal. 8:22-24, 28) [Julai 6, w05 7/1 uku. 30 fu. 3]
Mfano wa Daudi wa kutembea kwa “utimilifu wa moyo” unatuchocheaje kufanya vivyo hivyo? (1 Fal. 9:4) [Julai 13, w12 11/15 uku. 7 fu. 18-19]
Tunajifunza somo gani muhimu kutokana na simulizi linalohusu Yehova kumtuma Eliya kwa mjane wa Sarefathi? (1 Fal. 17:8-14) [Julai 27, w14 2/15 uku. 14]
Kutafakari simulizi la 1 Wafalme 17:10-16 kunawezaje kuimarisha azimio letu la kumtegemea Yehova kabisa? [Julai 27, w14 2/15 uku. 13-15]
Tunaweza kunufaikaje kutokana na mfano wa Eliya wa jinsi alivyokabiliana na hisia za kukata tamaa? (1 Fal. 19:4) [Ago. 3, ia uku. 102-103 fu. 10-12; w14 3/15 uku. 15 fu. 15-16]
Yehova alitendaje alipomwona nabii wake mwaminifu Eliya akiwa ameshuka moyo, na tunawezaje kumwiga Mungu wetu mwenye upendo? (1 Fal. 19:7, 8) [Ago. 3, w14 6/15 uku. 27 fu. 15-16]
Mfalme Ahabu alikuwa na maoni gani yasiyofaa, na Wakristo leo wanawezaje kuepuka kuwa na maoni kama hayo? [Ago. 10, lv uku. 164-165, sanduku; w14 2/1 uku. 14-15 fu. 3-4]
Tunaweza kujifunza nini kutokana na ombi la Elisha kwa Eliya, na hilo linawezaje kutusaidia tunapopata mgawo mpya katika kazi ya Ufalme? (2 Fal. 2:9, 10) [Ago. 17, w03 11/1 uku. 31 fu. 5-6]
Vijana wanawezaje kuiga imani na ujasiri wa msichana mdogo Mwisraeli anayetajwa katika 2 Wafalme 5:1-3? [Ago. 24, w12 2/15 uku. 12-13 fu. 11]
Yehu alikuwa na sifa gani ambazo watumishi wote wa Yehova wanapaswa kujitahidi kuiga katika siku hizi za mwisho? (2 Fal. 10:16) [Ago. 31, w11 11/15 uku. 5 fu. 4]